Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Hapa na Pale

Baraza la Usalama alasiri lilizingatia ripoti ya karibuni ya KM kuhusu maendeleo kwenye utekelezaji wa mapendekezo ya azimio 1701 katika Lebanon. Mratibu Maalumu wa UM kwa Lebanon, Michael Williams aliwapatia wajumbe wa Baraza taarifa yake kuhusu hali halisi Lebanon. Kadhalika Baraza la Usalama lilikuwa na mazungumzo ya hadhara kuhusu hali ya marekibisho Kosovo.

Hapa na Pale

John Holmes, KM Mdogo juu ya Masuala ya Kiutu na Mshauri wa UM Kuhusu Misaada ya Dharura Ijumanne ameanza ziara ya siku sita katika Sudan. Alizuru kambi ya Kalma, iliopo Nyala, Darfur Kusini yalipo makazi ya muda kwa wahamiaji wa ndani 88,000. Alipata fursa ya kuzungumza nawo na walimwomba wapatiwe hifadhi ziada kutoka vikosi mseto vya ulinzi amani vya UM na UA kwa Darfur, yaani vikosi vya UNAMID ambavyo polisi wake wanaendeleza doria ya kulinda kambi hizo kwa saa ishirini nanne mfululizo.