Usalama ni jambo linaloendelea kutia hofu Darfur:UM
Usalama unasalia kuwa jambo linalopewa kipaumbele cha kwanza na vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa na muungano wa Afrika Darfur UNAMID amesema mkuu wa mpango huo Ibrahim Gambari.
Usalama unasalia kuwa jambo linalopewa kipaumbele cha kwanza na vikosi vya kulinda amani vya Umoja wa Mataifa na muungano wa Afrika Darfur UNAMID amesema mkuu wa mpango huo Ibrahim Gambari.
Umoja wa Mataifa pamoja na serikali ya Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo watafanya mkutano juma lijalo kujadili njia za kulinda sehemu tano zilizo kwenye orodha ya sehemu za kiasili duniani ambazo ziko kwenye hatari ya kuangamia.
Idadi ya wakimbizi wa Sri Lanka wanaotaka kurejea nyumbani tangu kumalizika kwa vita mwaka 2009 inaongezeka limesema shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR.
Wakati Sudan Kusini inajiandaa kupiga kura ya maoni mwishoni mwa wiki hii, shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula WFP linajitahidi kuhakikisha kura hiyo ya kihistoria haita changia njaa zaidi katika eneo hilo ambalo limeghubikwa na miongo ya vita na majanga ya asili.
Hali ya kisiasa Nepal bado ni ya kutia mashaka, wakati vikosi vya kulinda amani vya UM vikijiandaa kuondoka.
Zikiwa zimesalia siku mbili kabla ya wananchi wa Sudan Kusini kuanza kupiga kura ya maoni ya kuamua hatma yao hapo siku ya Jumapili ijayo, mkuu wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Navi Pillay ameutaka uongozi wa Sudan kuhakikisha kura ya maoni inakuwa huru na ya haki.
Mgombea wa upinzani aliyetangazwa mshindi katika uchaguzi wa Novemba mwaka jana na kuzua utata nchini Ivory Coast Alassane Ouattara amesema ana imani suluhu ya mzozo wa kisiasa nchini humo itapatikana hivi karibuni.
Taarifa iliyotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu OCHA inasema machafuko katika mji wa Magharibi wa Duekoue nchini Ivory Coast kati ya jamii za kikabila za Malinke na Guere yanaendelea.
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia Balozi Augustine Mahiga amefanya ziara ya ghafla Moghadishu Somalia.
Mfanyakazi wa mpango wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika Darfur Sudan UNAMID ameachiliwa huru baada ya kushikiliwa mateka kwa siku 90.