Wabunge wa Somalia wampinga mwakilishi wa UM
Takribani wabunge 100 wa serikali ya mpito ya Somalia mwishoni mwa wiki wamefanya mkutano mjini Moghadishu na kumshutumu mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini humo Balozi Augustine Mahiga kuwa anasambaratisha serikali ya mpito.