Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wabunge wa Somalia wampinga mwakilishi wa UM

Takribani wabunge 100 wa serikali ya mpito ya Somalia mwishoni mwa wiki wamefanya mkutano mjini Moghadishu na kumshutumu mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa nchini humo Balozi Augustine Mahiga kuwa anasambaratisha serikali ya mpito.

Radio ya UM ni chombo muhimu kwa dunia:Wasikilizaji DRC

Tangu mapema miaka ya 1950 ilipoanzishwa Idhaa ya Kiswahili ya Radio ya Umoja wa Mataifa imekuwa msitari wa mbele sio tuu kujulisha ulimwengu shughuli za Umoja wa Mataifa na mashirika yake bali pia kuelimisha, kuhabarisha, kuburudisha, kutoa msaada na hata kuwapa fursa wasikilizaji kutoa maoni na madukuduku yao kuhusu Umoja wa Mataifa.