Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Dkt. Venance Shillingi, Mhadhiri Mwandamizi kutoka Chuo Kikuu Mzumbe nchini Tanzania akizungumza na Idhaa ya Umoja wa Mataifa kando mwa mkutano wa UN na wanazuoni uliofanyika New York, kuanzia Desemba 5-7 2023.
UN/Assumpta Massoi

Ni kwa vipi mfumo wa wamasai kujikwamua unaweza kuwa mfano kwa wengine Afrika?

Kitendo cha kabila la jamii ya wamasai kuweza kujimudu na maisha hata baada ya ukame uliosababishwa na mabadiliko ya tabianchi kuvuruga upatikanaji wa malisho kwa ajili ya mifugo yao kimeonekana kama moja ya mbinu mujarabu zinazoweza kusaidia nchi za Afrika kujengea mnepo wananchi wapo pindi mbinu walizozoea kujipatia kipato zinapovurugika.

Malori yaliyosheheni msaada wa kibinadamu yakijiandaa kuingia Gaza kupitia kivuko cha Rafah
© UNICEF/Eyad El Baba

Mashirika ya UN yaomba kufunguliwe njia nyingine ya kufikisha misaada Gaza

Zikiwa ni zaidi ya siku 100 tangu kuibuka upya kwa mzozo huko Mashariki ya Kati, mashirika ya Umoja wa Mataifa hii leo yametoa taarifa inayoelezea kuongezeka kwa hatari ya baa la njaa na milipuko ya magonjwa ya kuambukiza huku yakisisitiza muarobaini pekee kwa sasa ni kuruhusu njia mpya za kuingiza misaada ya kwenda kutatua changamoto zinazowakabili wananchi walioko Gaza. 

Sauti
3'34"
Watu waliojeruhiwa wakisubiri kutibiwa katika hospitali ya Al Shifa mjini Gaza. (Maktaba)
© WHO

Mzozo Gaza: Hospitali zazidi kuzidiwa uwezo, wagonjwa sakafuni

Ikiwa leo ni siku ya 93 tangu mapigano yaanze huko Ukanda wa Gaza kati ya jeshi la Israel na wanamgambo wa kipalestina waliojihami, likiwemo kundi la Hamas, mashirika ya Umoja wa Mataifa ya usaidizi wa kiutu yanazungumzia uwepo wa idadi kubwa ya vifo miongoni mwa wanawake na watoto huku yakisihi timu za madaktari ziruhusiwe kuingia eneo la Gaza ili ziendelee na jukumu la kuokoa maisha. 

Audio Duration
2'16"
Bendera ya Umoja wa Mataifa ikikabidhiwa kwa maafisa wa MONUSCO nchini DRC kuashiria kufungwa kwa ofisi ndogo za ujumbe huo wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani kwenye eneo hilo lililoko kilometa takribani 140 kutoka mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini.
UN/George Musubao

Ofisi ya MONUSCO Lubero, Kivu Kaskazini yafungwa

DRC, MONUSCO umefunga kituo chake kilichoko Lubero jimboni Kivu Kaskazini baada ya kuweko huko kwa miaka 21.Hatua hii ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wake wa kujiondoa kwa utaratibu kutoka DRC, kwa mujibu wa azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kufuatia ombi la serikali ya DRC.

Ngor Matiang, Mchezaji wa mpira wa Kikapu ambaye pia ni mwanafunzi kutoka Sudan Kusini.
UN News/Thelma Mwadzaya

Mpira wa kikapu unachangia amani, maendeleo na ustawi wa jamii

Kwa mara ya kwanza, Umoja wa Mataifa unaadhimisha siku maalum ya mpira wa kikapu ili kutambua mchango wake katika kuleta amani, maendeleo na ustawi wa jamii. Michezo, sanaa na mazoezi yana uwezo wa kubadili mitazamo, tabia, kadhalika kuhamasisha kuondoa vikwazo vya tofauti za rangi na siasa, kupambana na unyanyapaa na pia kumaliza ghasia. Kama michezo miengine ile, mpira wa kikapu unavuka mipaka yote, tamaduni na lugha. Ni kiunganishi kinachowaleta pamoja watu wa asili tofauti kutangamana, kujuana na hatimaye kuchangia kudumisha amani.

Afisa Habari wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO ofisi ya Beni jimboni Kivu Kaskazini akipatia mafunzo wanahabari, wanaharakati na wanafunzi wa Vyuo Vikuu kuhusu habari potofu na habari za uongo mjini Beni.
UN./George Musubao

MONUSCO imetuepusha kutumbukia kwenye usambazaji wa habari za uongo na potofu- Wanufaika

Kesho nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ni uchaguzi mkuu ikiwa ni tamati ya kampeni huku Umoja wa Mataifa kupitia ujumbe wake wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO umeshiriki kwa kusafirisha sio tu vifaa vya uchaguzi lakini pia kuelimisha wananchi jinsi ya kukabili na kuzia habari potofu na za uongo kwani ni tisho la amani na usalama.