Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Bendera ya Umoja wa Mataifa ikikabidhiwa kwa maafisa wa MONUSCO nchini DRC kuashiria kufungwa kwa ofisi ndogo za ujumbe huo wa Umoja wa Mataifa wa Kulinda amani kwenye eneo hilo lililoko kilometa takribani 140 kutoka mji wa Beni jimboni Kivu Kaskazini.
UN/George Musubao

Ofisi ya MONUSCO Lubero, Kivu Kaskazini yafungwa

DRC, MONUSCO umefunga kituo chake kilichoko Lubero jimboni Kivu Kaskazini baada ya kuweko huko kwa miaka 21.Hatua hii ni sehemu ya utekelezaji wa mpango wake wa kujiondoa kwa utaratibu kutoka DRC, kwa mujibu wa azimio la Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kufuatia ombi la serikali ya DRC.

Ngor Matiang, Mchezaji wa mpira wa Kikapu ambaye pia ni mwanafunzi kutoka Sudan Kusini.
UN News/Thelma Mwadzaya

Mpira wa kikapu unachangia amani, maendeleo na ustawi wa jamii

Kwa mara ya kwanza, Umoja wa Mataifa unaadhimisha siku maalum ya mpira wa kikapu ili kutambua mchango wake katika kuleta amani, maendeleo na ustawi wa jamii. Michezo, sanaa na mazoezi yana uwezo wa kubadili mitazamo, tabia, kadhalika kuhamasisha kuondoa vikwazo vya tofauti za rangi na siasa, kupambana na unyanyapaa na pia kumaliza ghasia. Kama michezo miengine ile, mpira wa kikapu unavuka mipaka yote, tamaduni na lugha. Ni kiunganishi kinachowaleta pamoja watu wa asili tofauti kutangamana, kujuana na hatimaye kuchangia kudumisha amani.

Afisa Habari wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini DRC, MONUSCO ofisi ya Beni jimboni Kivu Kaskazini akipatia mafunzo wanahabari, wanaharakati na wanafunzi wa Vyuo Vikuu kuhusu habari potofu na habari za uongo mjini Beni.
UN./George Musubao

MONUSCO imetuepusha kutumbukia kwenye usambazaji wa habari za uongo na potofu- Wanufaika

Kesho nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ni uchaguzi mkuu ikiwa ni tamati ya kampeni huku Umoja wa Mataifa kupitia ujumbe wake wa kulinda amani nchini humo, MONUSCO umeshiriki kwa kusafirisha sio tu vifaa vya uchaguzi lakini pia kuelimisha wananchi jinsi ya kukabili na kuzia habari potofu na za uongo kwani ni tisho la amani na usalama. 

Lilly Kiden akibeba mazao ya mbogamboga kutoka kwa shamba lake.
FAO

Asante FAO kunijengea mnepo sasa najikimu mimi na familia yangu: Lilly Kiden

Wakati mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi COP28 ukijiandaa kufunga pazia hapo kesho nakupeleka Sudan Kusini jimbo la Equatorial Mashariki ambako wakulima walioathirika na mabadiliko ya tabianchi sasa wanajengewa mnepo na mradi wa shirika la Umoja wa Mataifa la chakula na kilimo FAO na wengi wameweza kujikwamua pamoja na familia zao. Ungana na Flora Nducha akikuletea safari ya mafanikio ya mmoja wa wanuafa wa mradi huo wa FAO. 

Sauti
2'8"