Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Oscar Kalere Oscar, mhamiaji kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, na anaaishi nchini Tanzania tangu mwaka 2002 na sasa anafanya kazi ya uchungaji.
UN News

Asante Umoja wa Mataifa kupitia uhamiaji sasa nina familia Tanzania- Oscar

Ikiwa ni siku chache zimepita tangu dunia kuadhimisha siku ya wahamiaji duniani, Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la uhamiaji, IOM,  ukitoa wito kwa jamii ya kimataifa na nchi wanachama wa Umoja huo  kushiriki katika kufanikisha uhamiaji wa wale wanaokimbia ghasia makwao na halikadhalika wale wanaosaka fursa bora, mmoja wa wanufaika wa uhamiaji ametoa shukrani zake kwa taifa ambalo limempatia hifadhi baada ya kukimbia Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.

Jengo la dawati la jinsia na watoto kwa ajili ya kupinga na kutokomeza ukatili wa kijinsia na mila kandamizi dhidi ya wanawake na wasichana
Picha: UNFPA/Warren Bright

UNFPA Tanzania yakabidhi msaada wa dawati la jinsia wilayani Simanjiro

Shirika la Umoja wa Mataifa la idadi ya watu duniani na masuala ya afya ya uzazi UNFPA nchini Tanzania limekabidhi jeshi la polisi mkoani Manyara msaada wa jengo la dawati la jinsia na watoto ikiwa njia moja wapo ya jitihada za kupinga na kutokomeza ukatili wa kijinsia na mila kandamizi dhidi ya wanawake, wasichana na watoto.

Sauti
4'59"
Luteni Kanali Amin Stevin Mshana (katikati), Mkuu wa TANZBATT 6 akiwasili Berbérati, Mambéré-Kadéï, Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR.
TANZBATT 6/Kapteni Mwijage Inyoma

TANBAT 5 yakabidhi jukumu la ulinzi wa amani wa UN kwa TANBAT 6 nchini CAR

Kikosi cha 5 cha walinda amani wa Umoja wa Mataifa kutoka Tanzania, TANBAT 5 kilichokuwa kinahudumu katika Ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, MINUSCA, kimekamilisha muda wake  na kukipisha kikosi kingine cha 6 nacho kutoka Tanzania, TANBAT 6 ambacho kitaendeleza jukumu hilo. Kutoka Berberat, Kapteni Mwijage Inyoma ni Afisa Habari wa TANBAT 6 ametuandalia taarifa hii. 

Sauti
2'35"
Msichana akinywa maji katika  bustani wa shule yake huko Goré, kusini mwa Chad.
© UNICEF/Frank Dejongh

WHO yatoa wito wa hatua za haraka kuhakikisha maji salama na usafi duniani kote

Kwa ushirikiano na ofisi ya Umoja wa Mataifa ya masuala ya maji UN Water, shirika la Umoja wa Mataifa la afya duniani WHO limechapisha utafiti kuhusu hatua za kuhakikisha lengo la maendeleo endelevu kuhusu maji SDG 6 zinahitaji kuharakishwa kwani ni 25% tu ya nchi zilizofanyiwa utafiti zinatarajiwa kufikia malengo ya usafi wa mazingira, mabadiliko ya tabianchi na majanga lazima yazingatiwe katika kuunda mifumo yenye mnepo. 

Charlotte Fatuma, mkimbizi kutoka DRC anaendesha duka kwenye kambi ya wakimbizi wa ndani ya Coranne nchini Msumbiji kutokana na umeme ambao umefanikishwa na mradi unaotekelezwa na UNHCR, Benki ya Dunia na Benki ya Maendeleo ya Afrika.
UNHCR Video

Utu na maendeleo vyakutanishwa Coranne na kuleta ustawi kwa wakimbizi na wenyeji

Charlotte Fatuma na Neema Cenga ni wakimbizi kutoka Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC na sasa wanaishi ukimbizini nchini Msumbiji katika jimbo la Nampula. Kwa sasa Charlotte ni mjasiriamali mwenye mafanikio makubwa, akiendesha biashara ya duka kwenye makazi ya wakimbizi ya Coranne huku Neema naye akijitahidi kulea na kusomesha watoto wake.  

Sauti
4'28"