Mwaka 2022 tuazimie kujikwamua kutoka majaribuni- Guterres
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametuma salamu za mwaka mpya wa 2022 akitaka dunia iazimie kwa pamoja mwaka huu mpya uwe wa kuondokana na majaribu yanayotarajia kuikumba.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametuma salamu za mwaka mpya wa 2022 akitaka dunia iazimie kwa pamoja mwaka huu mpya uwe wa kuondokana na majaribu yanayotarajia kuikumba.
Ikiwa leo ni siku ya mtoto duniani, shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto UNICEF limetumia siku ya leo kuonesha ni kwa jinsi gani vijana wameamua kuchukua hatua kusongesha haki za msingi za mtoto ambazo ni kuishi, kuendelezwa, kulindwa na kushirikishwa.
Ili kuudhibiti ugonjwa wa Covid-19 unaosababishwa na virusi vya Corona, serikali ya Uganda imeamua kushirikiana zaidi na wadau mbalimbali yakiwemo makampuni ya mawasiliano na yale ya vinywaji katika juhudi za kuimarisha chanjo. Je, kampeni hiyo inatekelezwaje? Na mtazamo wa Waganda kuhusu chanjo hiyo ukoje sasa? Hii hapa taarifa iliyoandaliwa na mwandishi wetu wa Uganda John Kibego.
Kijana Mtanzania mpigapicha za mazingira Imani Nsamila ametangazwa kuwa mshindi wa Tuzo za Vijana za EU GCCA+ zinazolenga kuwasaidia wanahabari wachanga, waandishi na wapiga picha kusimulia taarifa au simulizi zenye nguvu za tabianchi kote ulimwenguni.
Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa maendeleo UNDP leo limezindua kampeni mpya na ya aina yake kwa ajili ya kuchagiza hatua dhidi ya janga la mabadiliko ya tabianchi.
Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Amina J. Mohammed amesema licha ya ushirikiano wa kimataifa kusalia kuwa njia pekee ya kutatua changamoto zinazokabili dunia, bado dunia inahaha kusaka njia bora zaidi ya kutekeleza ushirikiano huo wa kimataifa kivitendo.
Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limekuwa na mjadala wa wazi kuhusu wanawake, amani na usalama ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema wakati umefika kwa baraza hilo kuonesha kwa vitendo uungaji wake mkono wa harakati za wanawake katika ujenzi na uendelezaji wa amani badala ya kusalia maneno matupu. Flora Nducha na maelezo zaidi.
Leo tarehe 16 mwezi Oktoba ni siku ya chakula duniani ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres, anasema siyo siku tu ya kukumbushana umuhimu wa chakula kwa kila mkazi wa dunia, bali ni siku ya kutoa wito wa kufanikisha uhakika wa kila mtu kuwa na chakula.
Taifa la Cameroon linapatikana kwenye pwani ya bahari ya Atlantiki katika kona ambako Afrika ya Kati na Magharibi zinakutana. Wareno katika safari zao zama hizo waliita eneo hilo “Rio dos Camarões” au “Mto wa Kamba” kutokana na kubaini uwepo wa kiwango kikubwa cha aina hiyo ya viumbe vya baharini.
Mradi wa kuelimisha kuhusu ongezeko la machafuko , kutokuwepo usalama na watu kutawanywa kwenye eneo la Sahel umefanya kutungwa wimbo mahsusi na mtunzi kutoka Mali Vieux Farka Touré na kuimbwa na wanamuziki mbalimbali wa eneo hilo.