Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Wahamiaji wakiandaa samaki kwa ajili ya mauzo katika soko moja mjini Dubai
ILO/Deloche P

Tunachopitia sasa kwenye COVID-19 wahamiaji hupitia kila uchao- Guterres

Ikiwa leo ni siku ya wahamiaji duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres amesema ni mwaka wa kutathmini jinsi janga la Corona au COVID-19 lilivyosababisha mamilioni ya watu kukumbwa na machungu ya kutengana na familia zao na kutokuwa na uhakika wa ajira, jambo ambalo limewapatia watu hisia halisi ambazo wahamiaji hukumbana nazo kila wakati kwenye maisha yao.
 

Walinda amani kutoka Tanzania na Indonesia wakikagua daraja.
TANZBATT 7/Ibrahim Mayambua

Tumejipanga ili kutoa mchango bora zaidi katika vikundi vipya vya ulinzi wa amani DRC- Meja Jenerali Kapinga

Wakati Tanzania ikijiandaa kupeleka kikosi chake katika vikundi vipya vitakavyokuwa na uwezo wa kuchukua hatua haraka zaidi kukabiliana na vitisho na hatimaye kuimarisha ulinzi wa raia nchini Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, DRC , chini ya bendera ya Umoja wa Mataifa, mkuu wa mafunzo na utendaji wa kivita wa jeshi la wananchi wa Tanzania, JWTZ amezungumzia kile ambacho watafanya ili utendaji wao uendane zaidi na mazingira. Tupate maelezo zaidi kutoka Luteni Issa Mwakalambo Afisa habari wa kikosi cha 7 cha Tanzania kwenye kikosi cha kujibu mashambulizi. FIB, cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani DRC, MONUSCO. 

Sauti
4'13"
Wanafunzi wakimwagilia mimea maji kwenye shule ya msingi Laos.
© FAO/Manan Vatsyayana

Bioanuwai ya udongo ina umuhimu mkubwa lakini mchango wake haujapewa uzito unaostahili-FAO 

Katika kuelekea siku ya udongo duniani hapo kesho Desemba 5 shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa FAO limesema bayonuai ya udongo ina jukumu muhimu la kuchagia katika uzalishaji wa chakula , kuimarisha lishe, kulinda afya ya binadamu, kupunguza uchafuzi wa mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi , lakini mchango wake mara nyingi haupewi uzito unaostahili.