Mwaka 2020 umetububujisha machozi, na kutupitisha kwenye majaribu, lakini 2021 kuna nuru- Guterres
COVID-19 imebadili maisha yetu na kuutumbukiza ulimwengu katika mateso na huzuni. Ndivyo alivyoanza ujumbe wake wa mwaka mpya 2020, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres, ujumbe alioutoa kwa njia ya video kutoka jijini New York, Marekani, makao makuu ya Umoja wa Mataifa.