Mtazamo wa Kimataifa Habari za kiutu

Chuja:

Habari Mpya

Kutoka kushoto: Bendera ya UN ikipepea New York; Naibu Katibu Mkuu akiwa na nakala ya ripoti ya  UNCTAD; Walinda amani wa UN; Katibu Mkuu akiwa na wanawake viongozi waandamizi wa UN
UN

Zilizovuma mwaka 2018

Mwaka 2018 ulighubikwa na changamoto nyingi hususan kwa nchi za Afrika, mizozo ikiendelea kukumba bara hilo sambamba na magonjwa. Hata hivyo kulikuwa na habari chanya, na kwa muhtasari tutaangazia pande zote za sarafu wakati huu ambapo tunafunga mwaka huu wa 2018.
 

Wakimbizi kutoka Iran, Venezuela, Syria, Afghanistan na Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR
UNHCR/UNICEF

Mkataba wa kimataifa wa wakimbizi kupitishwa leo

Hii leo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani, Baraza Kuu la chombo hicho litapitisha mkataba wa kimataifa wa wakimbizi na hivyo kusaidia kwa kiasi kikubwa wale wanaokimbia makwao na nchi zinazowahifadhi, ambazo mara nyingi ni zile maskini zaidi duniani. Siraj Kalyango na maelezo zaidi.
 

Kikao chamwisho cha mkutano wa COP24 Katowice, Poland,16 Disemba 2018.
UNFCCC/James Dowson

Baada ya vuta ni kuvute ya wiki mbili muafaka wafikiwa COP24

Baada ya wiki mbili za majadiliano ya makundi zaidi ya 200 yaliyokusanyika Katowice, Poland kwa ajili mkutano wa Umoja wa  Mataifa wa mabadiliko ya tabianchi , COP24 ,yameidhinisha  muongozo wa utekelezaji wa mkataba wa Paris wa mwaka 2015, wenye lengo la kupunguza ongezeko ka joto duniani kuwa nchini ya nyuzi joto 2 ikilinganishwa na viwango vya kabla ya wakati wa viwanda.

Katibu Mkuu wa UN António Guterres alipokuwa akizungumza hii leo tarehe 12 Desemba 2018 na wajumbe wanaoshiriki COP24 huko Katowice Poland
UNFCCC Secretariat/James Dowson

Guterres afananisha kutotimiza mkataba wa mabadiliko ya tabianchi na kujiua

Wakati ambapo majadiliano kuelekea mpango madhubuti wa utekelezaji wa mkataba wa Paris wa mabadiliko ya tabianchi wa mwaka 2015 yakiendelea kukumbwa na vikwazo, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres leo hii amerejea Katowice, Poland kuwapa changamoto zaidi ya viongozi 100 wa serikali ambao wanakutana katika mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabia nchi COP24 kufikia makubaliano na kuikamilisha kazi.

Mtafiti Rebecca Adami akiwa katika studio za UN News kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York Marekani.
UN News/Paulina Greer

Wanawake walikuwa na mchango mkubwa katika kuandikwa kwa tamko la haki za binadamu

Wiki ijayo, dunia itaadhimisha miaka 70 ya tamko la Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu. Ingawa historia ya dunia inaonekana kuwasahau wanawake, mtafiti wa masuala ya haki za binadamu Dkt Rebecca Adami katika kitabu chake cha ‘Wanawake na tamko la haki za binadamu’ anasema wanawake walikuwa na mchango mkubwa katika kuliandaa na kulitekeleza tamko hilo.