Habari Mpya

Kabla ya kukata msaada hatua dhidi ya mabadiliko ya tabianchi na magonjwa zichukuliwe:Lowcock

 Akitafakari miaka miine ya uongozi wake kama mratibu mkuu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa na mkuu wa OCHA, Mark Lowcok amesema ni jinsi gani watu zaidi na zaidi wanavyohitaji msaada wa kibinadamu kwa sababu ya vita, mabadiliko ya tabianchi na magonjwa kama mlipuko wa Ebola na janga la corona au COVID-19.

Mwendesha Mashtaka Mkuu Mpya wa ICC aapishwa Rasmi

“Naapa kwamba nitatekeleza majukumu yangu kwa Mamlaka yangu ya Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Kamosa ya Jinai kwa heshima, uaminifu, bila upendeleo na kwa dhamiri, nitaheshimu usiri kwenye kufanya uchunguzi na kuendesha mashtaka” kiapo cha Mkuu mpya wa ICC

 

Punguzeni Gharama ya utumaji fedha:Guterres

“Nawasihi wadau wote kuendelea na juhudi za kupunguza gharama za kuhamisha fedha duniani, gharama hizo zipungue na hata zikaribia sifuri, maana hii ni huduma muhimu sana, hasa kwa nchi zinazoendelea.”

Kauli za chuki zinaongezeka DRC, hatua zichukuliwe:Keita 

Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye pia ni mkuu wa mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo, MONUSCO, Bintou Keita, amelaani vikali kuenea kwa ujumbe unaochochea chuki, vurugu na uhasama baina ya jamii kwenye majimbo kadhaa ya nchi hiyo. 

Asilimia 99 ya Watoto Niger hawajui kusoma na kuandika:Benki ya Dunia

Ikiwa leo ni siku ya mtoto wa Afrika, ndoto za kutimiza ajenda ya bara hilo ya mwaka 2040 ya kuwa na bara la Afrika linalomfaa mtoto wa Afrika ikiwemo katika suala la kupata elimu, kwa Niger huenda lisitimie kwani asilimia 99 ya watoto wenye umri wa miaka 10 ni wajinga wa kutokujua kusoma na kuandika.

 

Teknolojia imetuokoa wakati wa COVID-19 kusaidia jamaa nyumbani:DKT.Minja

“Zile fedha ambazo tunazituma zinamchango mkubwa sana sio tu kwa familia hata kwa jamii nzima kwa ujumla kwa maana ya kiuchumi .”  Dkt. Frank Minja 

Utumaji fedha kimtandao ulinusuru familia za kijijini mwaka 2020 

Mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya kilimo, IFAD umesema ingawa kiwango cha wahamiaji kutuma fedha nyumbani kimtandao  wakati wa janga la ugonjwa wa Corona au COVID-19 mwaka 2020 kimeongezeka, bado kaya za vijijini zilishindwa kunufaika vyema na utumaji huo kutokana na kukosa miundombinu ya kidijitali ya kupokea fedha hizo. IFAD imesema hayo ikiwa leo ni siku ya kimataifa ya familia kutumiana fedha.

Dola Milioni 135 zatolewa na UN kusaidia wanaokabiliwa na Njaa

Umoja wa Mataifa umetoa dola milioni 135 kutoka kwenye Mfuko wake wa dharura (CERF) ili kuongezea kwenye shughuli za kibinaadamu katika nchi 12 barani Afrika, Amerika na Mashariki ya Kati, amesema Mratibu wa Mfuko huo Bwana Mark Lowcock akiwa mjini New York, Marekani.

 

Janga la COVID-19 limeongeza ukatili dhidi ya wazee: mtaalam wa UN aonya

Wakati mitazamo ya zamani kuhusu uzee tayari inadhoofisha uhuru wa wazee katika kufanya uchaguzi na maamuzi yao wenyewe, janga la COVID-19 limeleta zahma zaidi, dhuluma na kutelekezwa dhidi watu hao, ameonya leo mtaalam huru wa  haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa, katika ujumbe wake kuhusu Ulimwengu siku ya kimataifa ya uelimishaji kuhudu ukatili dhidi ya wazee.

Hatutoi Taarifa za wakimbizi kwa serikali ya Bangladesh bila ridhaa ya Wakimbizi wenyewe : UNHCR

Shirika la umoja wa Mataifa linaloshughulikia wakimbizi UNHCR kupitia tarifa yake kwa vyombo vya habari hii leo mjini Geneva Uswisi limesema halikusanyi taarifa za wakimbizi wa Rohingya waliopo Bangladesh na kuipa serikali bila idhini ya wakimbizi wenyewe na iwapo wakimbizi hao watakataa kutoa ruhusa basi watapatiwa mahitaji muhimu kama wale waliokubali bila kubaguliwa kwa aina yeyote.