Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC ambaye pia ni mkuu wa mpango wa Umoja wa Mataifa nchini humo, MONUSCO, Bintou Keita, amelaani vikali kuenea kwa ujumbe unaochochea chuki, vurugu na uhasama baina ya jamii kwenye majimbo kadhaa ya nchi hiyo.