Christian Balslev-Olesen, Mshauri Mkazi kwa Huduma za Kiutu Usomali aliwasilisha hadharani barua maalumu iliofafanua hali ya vurugu katika Usomali. Balslev-Olesen aliwatahadharisha viongozi wa Usomali na makundi yote husika na hali huko, ikijumuisha vikosi vya Ethiopia, kwamba wanawajibika, kwa kulingana na sheria za kiutu za kimataifa, kuheshimu haki za raia na wajitahidi kuchanganua ni nani raia na nani mpiganaji wakati wanapoendeleza operesheni zao.