Viongozi wa wenyeji wa asili walioshiriki kwenye mijadala ya kikao cha karibuni cha mwaka, cha Tume ya Kudumu ya UM juu ya Masuala ya Haki za Wenyeji wa Asili walisisitiza kwenye risala zao, kwa kauli moja, ya kwamba haiyafalii Mataifa Wanachama kuendelea kupoteza wakati katika kipindi cha kihistoria ambapo kunahitajika kuuidhinisha halan ule mwito wa Baraza la Haki za Binadamu wa kukomesha ubaguzi dhidi ya wenyeji wa asili, na kuupatia umma huu uliotengwa kijamii haki zao halali, hasa kwenye juhudi za kudhibiti na kutunza ardhi na rasilmali ziliopo kwenye maeneo yao.