Hatimaye mjadala mkuu wa mkutano wa 76 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, UNGA76 umefunga pazia leo Jumatatu katika makao makuu ya Umoja huo jijini New York, Marekani huku Rais wa Baraza hilo Abdullah Shahid akisema mkutano huo umefanyika kwa mafaniko makubwa katikati ya janga la Corona au COVID-19 huku akitaja sababu za mafanikio hayo kuwa ni hatua bora za kupunguza maambukizi na viwango vya juu vya chanjo.