Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na uhamiaji IOM kwa kushirikiana na serikali ya China leo wanatazamiwa kuendesha mafunzo ya siku tatu ambayo yanalenga kuwasaidia watu waliokumbwa na vitendo vya usafirishaji haramu wa binadamu
Baada ya ulimwengu kushuhudia hali ngumu ya kiuchumi iliyosababisha kukwama kwa miradi mingi ya kimaendeleo na wakati pia ulimengu ukiendelea kukumbwa na kupanda kwa gharama ya chakula na nishati kunahitajika kuchukuliwa hatua zitakazochangia zaidi katika maendeleo.
Shirika la chakula la Umoja wa Mataifa limesema leo kuwa litaongeza usambazaji wa chakula kwa mamia ya raia wa Ivory Coast ambao wameyakimbia makazi yao na kuingia nchi jirani ya Liberia kutokana na mkwamo wa kisiasa unaoendelea nchini humo.
Pande zinazozozana kuhusiana na eneo la Sahara Magharibi, zimeshindwa kuafikiana namna ya kutanzua mzozo huo wakati wajumbe wake walipokutana kwa majadiliano maalumu chini ya uratibu wa umoja wa mataifa.
Mtaalamu mmoja wa takwimu za jamii raia wa Iran anayeshughulikia masuala ya maendeleo na afya ya uzazi pamoja na taasi inayotoa mafunzo juu ya masula ya afya ya uzazi wameshinda tuzo la idadi ya watu la Umoja wa Mataiafa.
Afisa anayehusika na masuala ya uchumi na ya kijamii kwenye Umoja wa Mataifa amesema kuwa mkutano kuhusu maendeleo ambao utaandaliwa mjini Rio de Janeiro nchini Brazil mwaka ujao utatoa fursa nzuri ya kuwasaidia watu kutoka kwenye umaskini.
Katibu mkuu wa shirika la mpango wa chakula duniani WFP Josette Sheeran amewataja akina mama kama kiungo muhimu katika kukabiliana na tatizo la njaa duniani.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amewataka vijana ulimwenguni kote kutumia vyema fursa zinazopatikana kwenye teknolojia ya habari pamoja na internet kubuni mambo yatakayoleta manufaa kwa jamii na siyo vinginevyo kwani amesisitiza kuwa mitandao ya tovuti ni nyenzo yenye ushawishi mkubwa wa kuleta maendeleo.
Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada ya kibinadamu OCHA ametenga dola milioni tano kuanza juhudi za kuwasaidia watu wanaokimbia machafuko nchini Libya.