Shirika la Umoja wa Mataifa la mpango wa chakula duniani WFP nchini Rwanda, linaendesha programu ya chakula kutoka nyumbani kwenda shuleni, programu ambayo inatekeleza malengo 6 ya maendeleo endelevu, SDGs likiwemo namba 2 la kutokomeza njaa na hivyo kuwaacha wazazi na wanafunzi wakiwa na furaha.