Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya haki za binadamu nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo leo Ijumaa imechapisha ripoti ya matokeo ya awali ya uchunguzi dhiti ya ubakaji wa kundi kubwa la watu na ukiukaji wa haki za binadamu uliotekelezwa na makundi ya watu wenye silaha kwenye mkoa wa Walikale kati ya Julai 30 na Agosti pili mwaka huu.