Mkurugenzi mkuu wa mpango wa kupambana na HIV /UKIMWI wa Umoja wa Mataifa Michel Sidibe, amerudia kueleza tena haja ya Jumuia ya Kimataifa kutoa dola bilioni 10 zaidi kusaidia mataifa yanayohitaji ili kufikia malengo yao ya kuhakikisha kwamba mipango ya kuzuia, kutibu na kuhudumia wagonjwa wa Ukimwi inamfikia kila mtu duniani.