Makamu wa rais nchini sudan Ali Osman Mohamed Taha amesema kuwa watu wa kusini mwa Sudan watapiga kura kwa njia huru na yenye uwazi mwezi Januari mwaka ujao wakati watakapoamua ikiwa watajitenga na eneo la kaskazini au watabaki kuwa wananchi wa nchi moja , kulingana na makubalino ya mani ya CPA yaliyomaliza vita kati ya serikali ya kaskazini mwa Sudan na jeshi la SPLM lililo kusini.