Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi linaomba kiasi cha dola milioni 12.5 kusaidia watu wanaishi nje ya makambi rasmi nchini Haiti na wale waliokimbilia nchi jirani ya Jamuhuri ya Dominican.
Kiongozi wa zamani wa Bosnia Serbia Radovan Karadzic anakutana uso kwa uso na shahidi wa kwanza wa upande wa mashikata kwenye kesi ya mauaji ya kimbari inyomkabili.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limeilalamikia serikali ya Zambia kwa kuwarudisha makwao wakimbizi kutoka Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu OCHA inasema miezi mitatu baada ya tetemeko la ardhi nchini Haiti mamilioni ya watu wameshapata msaada muhimu.
Wawakilishi kutoka karibu nchi 50 wanakutana mjini Washington leo kwa ajili ya mkutano wa usalama wa nyuklia ulioandaliwa na Rais wa Marekani Barack Obama.
Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudia watoto UNICEF amesema kuongeza upimaji wa hiyari wa virusi vya HIV na elimu kwa umma kutasaidia kukabiliana na ukimwi nchini Zambia.