Wajumbe wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, wamepongeza uamuzi uliofikiwa Mei 27 2021, na viongozi wa nchi ya Somalia baada ya Waziri mkuu wa nchi hiyo Mohamed Hussein Roble kuitisha mkutano wa kutekeleza makubaliano waliyojiwekea September 17 juu ya kuwa na uchaguzi mkuu wa kihistoria.