Sauti za wanawake na wasichana na ujuzi katika sayansi, teknolojia na ubunifu ni muhimu katika kuleta suluhu katika dunia ya sasa ambayo inashuhudia mabadiliko ikiwemo mabadiliko haribifu, yanasisitiza mashirika ya Umoja wa Mataifa likiwemo lile la wanawawake yaani UN Women na lile la elimu, sayansi na utamaduni UNESCO.