Ujuzi katika sayansi, teknolojia, uhandisi na hisabati unachagiza ubunifu na ni muhimu katika kufikia malengo ya maendeleo endelevu, SDGs amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres hii leo katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya wanawake na wasichana katika sayansi.