Wakati wa janga la COVID-19 pengo la ukosefu wa usawa kati ya matajiri na maskini limeongezeka zaidi, halikadhalika umaskini, ikiwa ni mara ya kwanza katika miongo kadhaa. Katika sehemu hii ya pili ya mfululizo wa makala kuhusu jinsi COVID-19 imebadili dunia, tunaangazia jinsi janga hilo limerudisha nyuma juhudi za kujenga jamii zenye usawa zaidi.