The United Nations High Commissioner for Refugees (UNHCR), along with its humanitarian partners, today launched a $ 157 million fundraising drive to help more than a quarter of a million people affected by Boko Haram attacks in the basin. lake Chad.
Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya kibinadamu na msaada wa dharura, Ursula Mueller, amesema hali bado ni tete nchini Syria kufuatia mapigano ya wenyewe kwa wenyewe yaliyodumu kwa zaidi ya miaka saba sasa.
Kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa, kumeanza jukwaa la vijana kutoka nchi wanachama wa umoja huo, wakiweka bayana kile wanachoona ni muhimu kwa mustakhbali wao.
Kampeni kuhakikisha kwamba ukatili dhidi ya wanawake na wasichana zinashika kasi kila uchao katika zama hizi ambazo Umoja wa Mataifa na wadau wake wanataka kuona vitendo hivyo dhalimu vinatokomezwa.
Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa Kipalestina, UNRWA limezindua harambee ya kuchangisha fedha zaidi ya dola millioni 800 kwa wapalestina walioko katika eneo linalokaliwa la Gaza na ukingo wa magharibi wa mto Jordan. Taarifa zaidi na Assumpta Massoi.