Huku kukiwa hakuna dalili ya kukoma mapigano yanayoendelea sasa nchini Libya mamia kwa maelfu ya wakimbizi wameendelea kuondoka nchini humo jambo ambalo linazidisha haja ya hitajio la msaada wa dharura.
Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limeelezea hofu yake kufuatia mabadiliko yaliyofanyiwa sheria za uhamiaji nchini Austria zinazowanyima haki wahamiaji likisema kuwa iwapo zitatekelezwa zitakuwa na athari hususan kwa watoto.
Mkuu wa shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR Antonio Guterres amekamilisha ziara yake nchini Misri ambapo alikagua hatua zilizochukuliwa na shirika hilo katika kushughulikia hali iliyosababishwa na mapigano nchini Libya.
Mahakama yenye mamlaka zaidi kwenye Umoja wa Mataifa ICJ umetupilia mbali kesi iliyowasilishwa mbele yake na George ikiishtaki urusi na makundi mengine ya waasi kwa kuendesha mauaji ya kikabila kwa raia wake.
Shughuli za kusambaza chakula nchini Libya kupitia kwa shirika la mpango wa chakula duniani WFP zimewafikia zaidi ya watu 7000 ambao wamehama makwao kutoka mji wa Ajdabiya.
Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya ubaharia IMO amezindua kituo cha kwanza mjini Mombasa Kenya kati ya vitatu vya kushirikiana taarifa za kusaidia kupambana na uharamiakwenye bahari ya Hindi na pwani ya Aden.