Makamu wa Rais wa Marekani Kamala Harris akihutubia Kikao cha 65 cha kamisheni ya hali ya wanawake duniani CSW65 mjini New York Marekani, amesema "hali ya wanawake ni hadhi ya demokrasia," akiongeza kwamba Marekani imedhamiria kutekeleza maadili ya kidemokrasia yaliyoko katika Azimio la Ulimwengu haki za binadamu.