Baraza la Usalama limeidhinisha Alhamisi, kuongeza muda wa afisi ya Umoja wa Mataifa nchini Cote d\'Ivoire, UNOCI pamoja na ule wa vikosi vya Ufaransa vinavowasaidia, kwa miezi minne zaidi ili kusaidia kuandaa uchaguzi wa huru, haki na wazi katika taifa hilo la Afrika Magharibi.