Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres ametoa wito wa hatua za kukomesha ghasia na ukatili majumbani dhidi ya wanawake na wasichana, kufuatia ripoti kuwa vitendo hivyo vimeshamiri hivi sasa maeneo mbali mbali duniani baada ya serikali kutaka wananchi wasalie majumbani kuepusha kuenea kwa ugonjwa wa virusi vya Corona, au COVID-19.