Nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, CAR, ujumbe wa Umoja wa Mataifawa kuweka utulivu, MINUSCA unajivunia wanawake madereva ambao wamechukua jukumu la kusafirisha watendaji wake katika maeneo mbalimbali na hivyo kuondokana na fikra potofu ya kwamba kazi hiyo ni ya wanaume pekee. Assumpta Massoi ameandaa taarifa inayofafanua zaidi.