Tukiwa bado tuko katika mwezi wa wanawake ambao umekuwa na matukio kadhaa makubwa kama maadhimisho ya siku ya kimataifa ya wanawake duniani na siku ya majaji wanawake, wanawake wanajeshi walinda amani kutoka Tanzania wanaohudumu katika kikosi cha 5 kutoka Tanzania kinacholinda amani kupitia mpango wa Umoja wa Mataifa wa kulinda amani nchini Jamhuri ya Afrika ya Kati, MINUSCAR, wameushukuru Umoja wa Mataifa pamoja na Jeshi lao la Tanzania kwa kuzingatia usawa wa kijinsia katika mipango ya ulinzi wa amani.