Kuelekea siku ya walinda amani duniani kesho Mei 29, siku ambayo mwaka huu inamulika wanawake walinda amani wa Umoja wa Mataifa na mchango wao katika ujenzi wa amani ya kudumu, tunamulika askari wanawake wa Tanzania wanaohudumu katika kikosi cha saba cha kikosi cha kujibu mashambulizi, FIB cha ujumbe wa Umoja wa Mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, DRC.