Nchini Tanzania, shirika la mpango wa maendeleo la Umoja wa Mataifa, UNDP limewezesha chama cha wakulima wa mboga na matunda nchini humo, TAHA kusaidia wanachama wake kulima kilimo bora cha mazao hayo kupitia mashamba ya mfano na ya kisasa na sasa wanapata masoko nchi za nje.