Katibu Mkuu wa Umoja wa mataifa Ban Ki-moon ambaye anafuatilia kwa karibu hali ya Ivory Coast amesema anahofia machafuko yalivyoshika kasi nchini humo.
Mahakakama ya uhalifu wa kivita nchini Cambodia ambayo inaungwa mkono na Umoja wa Mataifa imekamilisha kusikiliza rufani ya watuhumiwa wa uhalifu uliofanywa wakati wa kiongozi wa zamani wa taifa hilo Khmer Rouge.
Serikali ya Kusini mwa Sudan imetakiwa kuweka mikakati ya kukabiliana na vitisho vinavyoharisha usalama wa eneo hilo, ambavyo vinaendeshwa na makundi ya askari waaasi.
Shirika la kuratibu masuala ya kibinadamu OCHA linasema kuwa idadi ya watu wanaohitaji misaada ya dharura ya chakula kwenye nchi za Afrika Mashariki imeongezeka kwa watu milioni mbili zaidi hadi watu milioni nane wakati nchi zinapoendelea kushuhudia hali ya ukame.
Ban Ki-moon atafanya ziara Jumatau katika chuo kikuu cha Pennsylvania katika jimbo la Philadelphia kuzindua kikao cha tano cha kongamano la wakuu wa vyuo vikuu, alisema msemaji wake.
Mwakilishi maalumu wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhuru wa kidini au imani Heiner Bielefeldt amepongeza mazingira ya uwazi na kuvumiliana nchini Paraguay katika ngazi ya jamii na serikali kwa ujumla.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon leo amezindua ofisi mpya za shirika la Umoja wa Mataifa la mazingira UNEP na shirika la makazi duniani UN-HABITAT mjini Nairobi Kenya.
Mionzi ya nyuklia inayoendelea kuvuja kwenye mtambo wa Fukushima Daiichi nchini Japan umewafanya maelfu ya raia wa nchi hiyo kusalia na wasiwasi wa afya zao.
Gharama kubwa za chakula zimezuia watu milioni 19.4 katika nchi za Asia -Pacific kujikwamua na umasikini mwaka jana imesema ripoti ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa leo.