Kampeni ya kimataifa ya Umoja wa Mataifa kutanabaisha umuhimu wa chanjo katika kuokoa maisha hususani ya watoto itamalizika Jumapili wiki hii baada ya wiki nzima iliyoambatana na chanjo, mafunzo, maonesho na mijadala duniani kote.
Baraza la usalama na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa pamoja wamelaani vikali mashambulio ya mabomu kwenye mhagawa mjini Marrakech nchini Morocco ambako watu takribani 20 wameuawa na wengine wengi kujeruhiwa.
Shirika la umoja wa mataifa linalohusika na uhamiaji IOM, linatazamiwa kuendelea utoaji huduma inayohusiana na masuala ya UKIMWI nchini Haiti katika kipindi chote cha mwaka huu 2011.
Shirika la umoja wa mataifa linalohusika na watoto UNICEF limeendelea na operesheni yake ya utoaji wa huduma za dharura katika eneo la Kaskazini mwa Namibia ambako mamia ya watu wako kwenye hali mbaya kufuatia mvua kubwa iliyosababisha mafuriko yasiyopata kushuhudiwa kwa miaka 120 iliyopita.
Shirika la Umoja wa Mataifa la makazi UN-HABITAT mwezi huu liliandaa mkutano wa kimataifa mjini Nairobi Kenya yaliko makao makuu ya shirika hilo na kuhudhuriwa na wakilishi kutoka nchi mbalimbali duniani.
Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM limewaokoa watoto 20 waliokuwa wakisafirishwa kinyume cha sheria kwenye ziwa Volta nchini Ghana uokoaji unaojiri wakati ufadhili wa mradi huo unapofikia kikomo mwaka huu.
Mkuu wa shirika la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa Navi Pillay amekamilisha ziara ya siku mbili nchini Mauritania ambapo alizungumzia changamoto za masuala ya haki binadamu zinazoikabili nchi hiyo na maafisa wa ngazi za juu serikalini pamoja na waakilishi wa mashirika ya umma.
Shirika la kuratibu masuala ya kibinadamu la Umoja wa Mataifa OCHA linasema kuwa maelfu ya watu kusini na magharibi mwa Ivory Coast wanahitaji zaidi misaada ya kibinadamu.
Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR limeelezea wasiwasi wake kutokana na kuendelea kuzorota kwa hali nchini Somalia suala ambalo limesababisha watu wengi zaidi kukimbia makwao.