Hii leo ikiwa ni siku ya wanawake duniani, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amesema janga la COVID-19 limefuta maendeleo ya miongo kuelekea usawa wa jinsia huku wanawake wakikumbwa zaidi na machungu, bado kundi hilo limesalia kuwa mstari wa mbele kwenye hatua dhidi ya janga la Corona.
Athari za janga la COVID-19 zinatishia maisha na haki za wakimbizi, wanawake na wasichana wasio na makazi, limeonya leo shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi NHCR, wakati ikiadjimishwa Siku ya wanawake duniani.
Licha ya serikali nyingi kote duniani kushirikiana katika kukabiliana na mlipuko wa COVID-19 mnano mwaka 2020, nchi nyingi na wananchi wake waliendelea kukosa usalama kutokana na vikundi vyenye itikadi kali.
Kuelekea siku ya wanawake duniani tarehe 8 mwezi huu wa Machi tunaelekea nchini Tanzaina ambako msichana mmoja mhitimu wa Chuo Kikuu amejikuta akiendeleza kipaji chake cha kuchora picha badala ya kubeba chaki kufundisha wanasayansi kutokana na ukosefu wa ajira, hatua ambayo imemfungulia milango mingi zaidi.