Leo kikao cha 54 cha wanawake kimeanza hapa mjini New York Marekani. Kikao hicho kinachohudhuriwa na maelfu ya wanawake kutoka sehemu mbalimbali duniani na mashirika ya Umoja wa Mataifa, kitatathmini ajenda za mkutano wa Beijing uliofanyika mika 15 iliyopita.