Umoja wa Mataifa na washirika wake wanapeleka misaada ya dharura kwa watu walioathirika na maporomoko ya ardhi yaliyotokana na hali mbaya ya hewa na mvua kubwa nchini Madagascar.
Taarifa ya pamoja iliyotolewa kwa ajili ya kuazimisha siku ya maji duniani itakayokuwa Jumatatu ijayo tarehe 22 Machi inasema maji safi ni haki ya kila mtoto.
Maafisa wa serikali ya Sudan leo wametia saini mkataba wa kusitisha vita kwa miezi mitatu na kundi lingine la waasi la Liberation and Justice Movement (LJM).
Ripoti iliyotolewa na shirika la Umoja wa Mataifa la makazi UN-HABITAT inayoelezea hali ya miji duniani kwa mwaka 2010/2011 inasema, watu milioni 227 wameepuka maisha ya mitaa ya mabanda katika muongo mmoja uliopita.
Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na idadi ya watu UNFPA linasema matatizo ya ukatili wa kimapenzi dhidi ya wanawake nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo ni makubwa na athari zake sio kwa wanawake tuu bali hata kwa jamii nzima.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amewasili mjini Moscow kwa ajili ya kufanya mazungumzo na viongozi wa Urusi kuhusu mahusiano katika muundo wa Umoja wa Mataifa.
Nchi ambazo zinahusika na uchafuzi wa mazingira kutokana na gesi ya viwandani kwa zaidi ya robo, sasa zimeamua kuunga mkono mkataba ulioafikiwa kwenye mkutano wa mwaka jana Copenhagen Denmark.
Ripoti ya kamati ya baraza la usalama kuhusu Somalia na Eritrea iliyowasilishwa leo inasema shughuli za kuleta amani na usalama nchini Somalia zinakabiliwa na vizingiti vingi ukiwemo ufisadi katika taasisi za serikali.