Rais wa mkutano wa 73 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa unaotamatishwa hii leo, María Fernanda Espinosa ametaja marufuku ya plastiki zinazotumiwa mara moja na kutupwa kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa jijini New York, Marekani kuwa moja ya mafanikio makubwa ya kipindi chake.