Leo dunia inaadhimisha siku ya usikivu wa masikio katika kipindi ambacho tayari ripoti mpya ya shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO imetahadharisha kuwa kufikia mwaka 2050 takribani watu bilioni 2.5 ulimwenguni watakuwa wanaishi na kiwango fulani cha kupoteza uwezo wao wa kusikia ikiwa hatua hazitachukuliwa mapema.
Misitu ni uhai na sio tu kwa binadamu na mazingira bali pia kwa asilimia 80 ya viumbe vyote vya porini, hivyo kutumia vyema na kuilinda ni kwa maslahi ya watu wote, sayari dunia na maendeleo amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres katika ujumbe wake wa siku ya wanyamapori duniani inayoadhimishwa leo.
Mkurugenzi mkuu mpya wa saba wa shirika la biashara duniani WTO, Ngozi Okonjo-Iweala ameanza kazi rasmi Jumatatu akiwa ni mwanamke na Mwafrika wa kwanza kushika wadhifa huo na ameahidi kufanya kila awezalo kuleta mabadiliko.
Taka za plastiki ni moja ya changamoto kubwa katika uhifadhi wa mazingira huku nchi zikifanya juhudi mbali mbali kukabiliana na changamoto hii kwani ina athari kwa viumbe na mazingira kwa ujumla.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres amehutubia mkutano wa Munich wa masuala ya usalama hususan vipaumbele vya hatua za kimataifa ambapo ametaja mambo makuu manne ya kuzingatia ili kuwezesha dunia kujikwamua salama kutoka athari za majanga yanayokumba dunia likiwemo lile la ugonjwa wa Corona au COVID-19 pamoja na mabadiliko ya tabianchi ambayo yanatishia amani na usalama na duniani.
Leo ni siku ya redio duniani, siku ambayo huadhimishwa kila tarehe 13 ya mwezi Februari kutoa fursa ya kuangazia mabadiliko, ubunifu na uunganishaji wa chombo hicho ambacho kimetimiza miaka 110.
Umoja wa Mataifa uko tayari kusimama na ikihitajika kuchangia katika uokoaji na juhudi za kusaidia kufuatia maporomoko ya theluji na mafuriko yalikumba maeneo ya kaskazini mwa India amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres Jumapili.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa António Guterres amemteua tena Michael Bloomberg wa Marekani kuwa mjumbe wake maalum wa hatua thabiti na zenye matamanio makubwa katika kukabili tabianchi.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres ameelaani vikali kushikiliwa kwa viongozi wa kisiasa na maafisa wa serikali ikiwemo kiongozi mkuu wa Myanmar Aung San Suu Kyi na rais Win Myint na jeshi la nchi hiyo.
Baraza la kiuchumi na kijamii la Umoja wa Mataifa ECOSOC leo limetuimiza miaka 75 tangu kuanzishwa kwake huku dunia na Umoja wa Mataifa wakikabiliwa na changamoto kubwa zaidi za kiuchumi na kijamii na hasa mgogoro wa kiafya wa janga la corona au COVID-19 kuwahi kushuhudiwa.