KM alipokuwa New Delhi, Bara Hindi Ijumaa aliwaambia waandishi habari kama katika siku mbili ziliopita alifanikiwa kufanya mazungumzo ya hali ya juu, ya ushauri juu ya hali katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (JKK), na Raisi Paul Kagame wa Rwanda, Raisi Joseph Kabila wa JKK na Raisi Jakaya Kikwete wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa UMwa Afrika. Kadhalika KM alisema alizungumza na Mwenyekiti wa Kamisheni ya Umoja wa Afrika, Jean Ping, Waziri wa Masuala ya Nchi za Kigeni wa Marekani, Condoleeza Rice,