Wakati serikali na mamilioni ya wananchi wa Uganda wakijiandaa kushiriki uchaguzi mkuu wa Rais na wabunge unaotarajiwa kufanyika kesho Alhamisi Januari 14, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ametoa wito kwa wadau wote nchini humo kuhakikisha demokrasia inachukua mkondo.