Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Tijjani Muhammad-Bande ambaye alichaguliwa kuchukua wadhifa huo mnamo mwezi Septemba mwaka jana 2019, hii leo jumatatu, awewasilisha kwa nchi wanachama, vipaumbele vyake vya mwaka 2020.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, António Guterres leo Jumatatu amesema migogoro ya mataifa inachangia katika nchi nyingi zaidi kuchukua uamuzi ambao matokeo yake hayatabiriki na yanazua hatari kubwa ya matokeo ya mipango mibovu.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres leo ameungana na dunia kuukaribisha mwaka mpya wa 2020 akiisihi dunia kudumisha amani hasa muongo wa utimizaji wa malengo ya maendeleo endelevu au SDGs ukianza.