Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, OHCHR kupitia taarifa iliyotolewa na msemaji wake Ravina Shamdasani mjini Geneva, Uswisi imesema inaguswa na vurugu na kile kinachosemwa kuwa ni ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Bangladesh kabla, wakati na baada ya uchaguzi uliofanyika tarehe 30 mwezi uliopita wa Desemba.