Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa akizungumza hii leo Jumatatu mjini Vienna Austria akiwa na Balozi wa amani wa Umoja wa Mataifa, mwanamuziki mcheza ‘Cello’ au Fidla, Yo-yo Ma, amesema kama lilivyo kundi la muziki mzuri, jamii zilizofanikiwa zina uwiano wa utofauti na utamaduni na hicho ni chanzo cha utajiri mkubwa na si tishio.