Shirika la mpango wa chakula duniani, WFP na shirikisho la soka duniani, FIFA wamekubaliana kutumia mpango wa mpira shuleni unaondesha na FIFA na ule wa mlo shuleni unaondeshwa na WFP, kuimarisha stadi za wanafunzi kama njia mojawapo ya kujenga jamii imara, endelevu na zenye ustawi.