KM Ban Ki-moon alifanyisha mkutano rasmi wa kwanza na wawakilishi wa vyombo vya habari vya kimataifa waliopo Makao Makuu ya UM mjini New York mnamo Alkhamisi ya tarehe 11 Januari 2007. KM Ban aliwafafanulia ratiba ya masuala aliyokabiliana nayo siku 10 baada ya kuchukua madaraka ya kuongoza taasisi hii muhimu ya kimataifa.
Januari 01, 2007 Ban Ki-moon, aliyekuwa Waziri wa Masuala ya Nchi za Kigeni wa Jamhuri ya Korea au Korea ya Kusini, alianza kazi rasmi kama ni KM wa nane wa Umoja wa Mataifa.