Ripoti ya mwezi Juni (2007) ya Shirika la UM juu ya Miradi ya Maendeleo (UNDP) ilibainisha mataifa ya Afrika yaliopo kusini ya Sahara bado yamepwelewa sana kwenye juhudi za maendeleo, kwa ujumla, na hakuna dalili haya yatafanikiwa kuyakamilisha, kwa wakati, yale Malengo ya Maendeleo ya Milenia (MDGs) ya kupunguza kwa nusu, kabla ya 2015, umasikini, njaa, maradhi na kutojua kusoma na kuandika.