Mapema wiki hii KM Ban Ki-moon alikutana na wajumbe wa Baraza la Usalama, kwenye kikao cha faragha, na walizingatia matokeo ya mazungumzo aliyokuwa nayo KM na viongozi wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (AU) walipokutana kwenye pambizo za Mkutano Mkuu uliofanyika karibuni katika mji wa Addis Ababa, Ethiopia.