Jumatano hii, kama ilivyo ada kila mwaka Februari 13, dunia inaadhimisha siku ya redio duniani ujumbe ukiwa majadiliano, uvumilivu na amani ambapo Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Antonio Guterres kupitia ujumbe wake kwa ulimwengu kuhusu siku hii amesema redio ni chombo chenye nguvu.