Mkutano wa 25 wa nchi wanachama wa mkataba wa kimataifa wa mabadiliko ya tabianchi, COP25 ukianza hii leo mjini Madrid, Hispania, Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Mpango wa mazingira wa Umoja wa Mataifa, UNEP Inger Andersen awali mjini New York Marekani kupitia mahojiano maalumu na UN News amesema moja ya vipaumbele vikuu vya mkutano huu itakuwa ni kufikia muafaka wa ibara ya sita ya mkataba wa Paris ambayo haikupata muafaka katika mkutano wa mwaka jana uliofanyika mjini Katowice Poland.